Jumapili hii katika Jukwaa la Michezo tunaangazia kuanza kwa michuano ya soka barani Afrika baina ya wachezaji wasiozidi miaka 20, mechi zimeanza nchini Senegal.Utasikia pia uchambuzi wa kombe la dunia kuhusu mchezo wa Cricktet katika michuano inayoendelea nchini New Zeland na Australia.
Vipindi vingine
-
Uganda : Uwanja wa Namboole kuanza kutumika kwa mechi za kufuzu Kombe la dunia
Tuliyokuandalia ni pamoja na Uchambuzi wa orodha ya mwisho ya Kikosi cha Marathon cha Team Kenya kuelekea Olimpiki, watu watano nchini Kenya wapigwa marufuku ya muda kwa madai ya upangaji mechi. Nchini Uganda, Rais wa FUFA asema uwanja wa Naambole utakuwa tayari kuandaa mechi wa kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026 na Ligi ya Basketboli barani Afrika mkondo wa Sahara umeanza leo.04/05/202423:54 -
KipKeino Classic: Mmarekani Kenneth Bednarek ashinda mbio za mita 100
Tuliyokuandalia hii leo ni pamoja na matokeo ya riadha za KipKeino Classic, uchambuzi wa debi la Tanzania na Mashemeji nchini Kenya, mabondia 11 wa DRC wafuzu nusu fainali ya michuano ya African Boxing Cup, matokeo ya ligi ya basketboli Afrika mkondo wa Nile na Ligi ya Mabingwa barani Ulaya20/04/202423:51 -
Olimpiki: Nigeria na Zambia zafuzu mashindano ya Olimpiki soka ya kina dada
Kwenye makala haya utasikiliza uchambuzi wa mechi za kufuzu soka ya kina dada Olimpiki na shirikisho la riadha duniani kuwa shirikisho la kwanza kutoa tuzo za fedha, maandalizi kuelekea riadha za KipKeino Classic, mkusanyiko wa michezo DRC, uchambuzi wa mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati Tiger Woods na Novak Djokovic waweka historia kubwa duniani kwenye gofu na tenisi mtawalia.13/04/202423:55 -
CAFCL:Simba na Yanga zabanduliwa michuano ya Klabu Bingwa Afrika
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na uchambuzi wa hatua ya robo fainali mkondo wa pili michuano ya Klabu Bingwa Afrika, matokeo ya kufuzu soka Olimpiki ya kina dada, mwanasoka wa Afrika Kusini kuuawa, PSG Academy yatoa mafunzo kwa makocha nchini Rwanda, Kenya yatangaza orodha yake ya wanariadha wa mbio za Marathon kwenye Olimpiki ya mwaka huu, Ufaransa na Kenya kushirikiana kujenga viwanja nane nayo PSG ikiwa tayari kutoa pauni milioni 111 kumsajili mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen06/04/202423:45 -
WRC Safari Rally Kenya : Mashindano ya mbio za magari yanaendelea nchini Kenya
Karibu katika makala jukwaa la michezo, leo hii tumekuandalia taarifa kadhaa kuanzia katika mashindano ya mbio za magari Safari rally nchini kenya, michuano ya klabu bingwa barani afrika Al Ahly wakiishinda Simba goli moja sifuri kisha Tp Mazembe kupata sare dhidi ya Petro Atletico ya Angola na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Sierra Leone Lamin Bangura afariki akiwa na umri wa miaka 59 katika ajali ya basi.30/03/202423:53