Pata taarifa kuu
UEFA

UEFA yasisitiza haihitaji teknolojia ya kubaini ikiwa mpira umevuka mstari

Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya Michel Platini amekariri msimamo wake wa hapo awali kuwa teknolojia mpya ya kubaini ikiwa mpira umevuka mstari au la usitumiwe katika mashindano ya UEFA.

Matangazo ya kibiashara

Majaribio ya teknolojia hiyo yameanza kutumiwa katika mashindano ya kutafuta bingwa wa klabu bora duniani yanayoendelea nchini Japan.

Platin ameongeza kuwa  ni afadhali kuwatumia marefarii  wanaosimama nyuma ya mlingoti ya magoli mfumo ambao UEFA  imekuwa ikitumia kuanzia mwaka 2009 kubaini ikiwa mpira umevuka mstari au la.

UEFA inasema itaigharimu Euro Milioni 50 kuweka mitambo hiyo ya teknolojia ikilinganishwa na ikiwa wangeajiri marefarii ambao gharama itakuwa ya chini .

Teknolojia ya The Hawk-Eye  itakuwa inatumia kati ya kamera sita na nane zitakazofungwa katika mlingoti ya magoli hayo huku ile nyingine ya GoalRef ikibaini ikiwa mpira utakuwa umevuka mstari.

FIFA inasema itatumia mfumo huo wakati wa mashindano ya kombe la dunia nchini Brazil mwaka 2014.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.