Upangaji wa timu kwenye makundi wakamilika Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Upangaji wa timu kwenye makundi kwa ajili ya ligi ya mabingwa barani Ulaya umekamilika jana Alhamisi jijini Monaco, huku jumla ya makundi nane yakipangwa kwa ajili ya michuano hiyo.
Imechapishwa:
Timu ya Montpellier, ambayo ndiyo timu bingwa ya Ufaransa itachuana na Arsenal katika kundi B huku mabingwa watetezi wa Ligi kuu ya Uingereza Manchester City watachuana na mshindi wa mara tisa wa mabingwa wa Ulaya Real Madrid.
Makundi mengine ni kama inavyoonekana hapa chini
Kundi A A: Porto, Dynamo Kiev, Paris St Germain, Dinamo Zagreb
Kundi B: Arsenal, Schalke, Olympiakos, Montpellier
Kundi C: AC Milan, Zenit St Petersburg, Anderlecht, Malaga
Kundi D: Real Madrid, Manchester City, Ajax, Borussia Dortmund
Kundi E: Chelsea, Shakhtar Donetsk, Juventus, FC Nordsjaelland
Kundi F: Bayern Munich, Valencia, Lille, BATE Borisov
Kundi G: Barcelona, Benfica, Spartak Moscow, Celtic
Kundi H: Manchester United, Braga, Galatasaray, CFR Cluj
Ligi ya mabingwa barani Ulaya inataraji kuanza tarehe 18 na 19 September.