Cote d'Ivoire yafuzu kucheza kombe la mataifa Afrika 2012 Gabon na Equitorial Guinea.
Ivory Coast imefuzu katika mashndano ya kuwania ubingwa wa Afrika katika mchezo wa soka,baada ya kuichabanga Benin mabao 6-2 katika mchuano wa kufuzu wa mashindano hayo,na hivyo inaongoza kundi hilo kwa alama 12.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Alama hizo kwa sasa haziwezi kufikiwa na timu yeyote katika kundi hilo,hasa baada ya Burundi kuisadia the Elephantys kufuzu mapema kwa kuwashinda Rwanda mabao 3-1,jijini Bunjumbura.
Tayari nchi wenyeji Equatorial Guinea na Gabon wamefuzu pamoja na nchi ya Botswana.
Uganda Cranes,nao wanahitaji sare au ushindi mmoja kujihakikishia naafasi yao katika kinyanyoro hicho lakini mamabo yalivyo kwa sasa,iushindi wao wa mabao 2-1 dhidi ya Guinea Bissau jijini Kampala umefanaya vijana wa Uganda kuwa mguu moja huko Gabon.
Timu za Kenya na Tanzinia nazo zinahitaji muujiza kufuzu kwa fainali hizo,baada ya kushindwa ugenini.Harambee Stars ya Kenya ilifungwa na wenyeji wao Angola bao 1 kwa 0,huku Taiafa stars ya Tanzania wakilazwa na Jamhuri ya Kati mjini Bangui mabao 2 kwa 1.
Ifuatayo ni orodha kamili ya matokeo na msimamo wa makundi:-
Ijumaa, Juni 3 - Ghana 3-1 Congo
Jumamosi , Juni 4 Zambia 3-0 Mozambique - Uganda 2-0 Guinea Bissau- Namibia 1-4 Burkina Faso - Cameroon 0-0 Senegal - Sierra Leone 1-0 Niger - Morocco 4-0 Algeria
Jumapili, Juni 5 - Mauritius 1-2 DR Congo - Zimbabwe 2-1 Mali - Ethiopia 2-2 Nigeria - Swaziland 1-2 Sudan - Botswana 0-0 Malawi - Burundi 3-1 Rwanda - Comoros 1-1 Libya - Angola 1-0 Kenya - Central African Republic 2-1 Tanzania - Benin 2-6 Cote d’Ivoire - Liberia 1-0 Cape Verde Islands - Guinea 4-1 Madagascar - Tunisia 5-0 Chad - Egypt 0-0 South Africa.
Zaidi:www.cafonline.com/