Pata taarifa kuu
UFARANSA-LEBANON

Emmanuel Macron aahidi euro milioni 100 kusaidia raia wa Lebanon

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameahidi kuwa serikali yake itatoa Euro Milioni 100 kama msaada wa dharura kwa nchi ya Lebanon, lakini pia dozi  500,000 za kukabiliana na janga la Covid-19.

Rais wa Ufaransa, akifungua mkutano wa 3 wa kimataifa kuhusu Lebanon kupitia njia ya video, akiwa mji wa Fort de Brégançon, huko Var (kusini-mashariki mwa Ufaransa).
Rais wa Ufaransa, akifungua mkutano wa 3 wa kimataifa kuhusu Lebanon kupitia njia ya video, akiwa mji wa Fort de Brégançon, huko Var (kusini-mashariki mwa Ufaransa). AFP - CHRISTOPHE SIMON
Matangazo ya kibiashara

Rais Macron ametoa ahadi hiyo, katika kongamano la Kimataifa kuisaidia Lebanon kupata Dola Milioni 350 kulisaidia taifa hilo kuinuka kiuchumi.

Mwaka mmoja baada ya shambulio kwenye bandari ya Lebanon, nchi hiyo imekuwa katika kipindi kigumu cha kiuchumi, lakini pia imekuwa ikishuhudia changamoto za kisiasa.

Msaada huu utajikita hasa katika elimu, mahitaji ya chakula na kilimo, ametangaza rais wa Ufaransa, kwa kufungua mkutano huo kupitia njia ya video, akiwa mji wa Fort de Brégançon, huko Var (kusini-mashariki mwa Ufaransa). Mkutano ambao unafanyika kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa, mwaka mmoja baada ya mlipuko kwenye bandari ya Beirut.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.