Wimbi la Siasa
Sudan: Majenerali waendelea kupimana nguvu licha ya juhudi za kidiplomasia
Imechapishwa:
Cheza - 10:00
Wiki hii kwenye Makala wimbi la siasa, Jupiter Mayaka anafanya mwendelezo wa mzozo unaoendelea nchini Sudan, wakati huu hali ya kibinadamu ikizidi kuwa mbaya, kutokana na raia kuuawa na misaada kutowafikia waathiriwa.
Matangazo ya kibiashara
Juhudi za kidiplomasia zinaendelea kutoka ukanda na kimataifa, ili kuwapatanisha mkuu wa jeshi la Sudan, jenerali Abdel Fattah al-Burhan na naibu wake, Mohammed Hamdan Daglo maarufu Hemedti ambaye ni kiongozi wa kikosi cha RSF.