Leo tunatupia jicho nafasi ya wanawake kwenye siasa za bara Afrika. Wiki hii siku ya Jumapili tarehe 19 rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, anatimiza miaka mitatu madarakani, baada ya kuapishwa kuongoza nchi hiyo kama rais wa sita, na kuwa rais wa kwanza mwanamke.
Samia alichukua hatamu za uongozi baada ya kifo cha mtangulizi wake John Magufuli.
Huku nchini Namibia, chama tawala SWAPO, kimemteua mwanamke mwingine Netumbo Nandi-Ndaitwah kuwa mgombea wake wakati wa uchaguzi huu mwaka ujao.
Je, nyota ya wanawake barani Afrika, kwenye medani ya kisiasa imeanza kungaa?
Kujadili hili, tunaungana nayeAnna Henga Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu akiwa Dar es salaam nchini Tanzania na Maimuna Mwidau akiwa Mombasa akiwa Kenya.