Milipuko ya Kipindu pindu na ukakamavu wa wanawake wa Malawi kupata tiba ya saratani
Imechapishwa:
Mlipuko wa Kipindu Pindu unazidi kuwa pasua kichwa kwa mataifa ya Afrika ya Kusini ikiwemo Zambia na Zimbabwe.Na katika mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya uzazi,wanawake kutoka Malawi hulazimika kusafiri hadi Kenya kupata matibabu ya Radiotherapy
Zambia inaendelea kutekeleza masharti makali kupambana na mlipuko hatari wa Kipindu pindu ambao unazidi kusababisho vifo vya wengi.
Shirika la afya duniani ,WHO limetoa dozi milioni 1.6 ambazo zitasambazwa kutumika katika mikoa iliyoathirika ikiwemo Lusaka.
Na januari dunia inapoungana kutoa uhamasisho kuhusu saratani ya shingo ya uzazi ambayo inasababisha vifo vingi miongoni mwa wanawake ,tunakuletea simulizi ya wanawake kutoka Malawi ambao hufunga safari hadi Nairobi kutafuta matibabu ya Radiotherapy ambayo bado haipatikani nchini mwao.