Wimbi la Siasa
Hofu ya wizi wa kura yaanza kutanda kwenye Vichwa vya Wagombea Urais nchini Kenya huku sera ya ardhi ikiendelea kuwa tete
Imechapishwa:
Cheza - 09:56
Wananchi wa Kenya wanatarajiwa kupiga kura kuchagua viongozi mbalimbali akiwemo Rais katika ucgaguzi unaotarajiwa kufanyika Machi 4 mwaka huu. Yapo masuala mengi yanayofanyika wakati wa mchakato wa uchaguzi unaendelea ikiwa ni pamoja na wagombea kuendelea kunadi sera zao.Makala ya Wimbi la Siasa juma hili inaangazia suala la hofu ya wizi wa kura inayoonyeshwa na wanasiasa nchini Kenya lakini pia suala la ardhi ambalo linatajwa kuwa chanzo cha vurugu na namna gani liangaliwe ili kuepusha machafuko ya baada ya uchaguzi mwaka 2007.