Pata taarifa kuu
MEXICO

Rais mpya wa Mexico Enrique Pena Nieto aapishwa, vurugu zatawala kupinga zoezi hilo

Takribani watu 25 wamejeruhiwa katika vurugu kati ya polisi na waandamaji wanaopinga kuapishwa kwa rais mpya wa Mexico Enrique Pena Nieto ambaye alipata ushindi katika uchaguzi wa mwezi julai mwaka huu.

Reuters
Matangazo ya kibiashara

Muda mchache baada ya kuapishwa Rais Pena Nieto alitoa hotuba ambapo ameahidi kuimarisha usalama na uchumi katika nchi hiyo.

Sherehe za kuapushwa kwa rais huyo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kimataifa akiwepo makamu wa rais wa Marekani Joe Biden.

Pena Nito aliibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake wa karibu Andre Manuel Lopez Obrador ambaye alipinga matokeo hayo na kudai mpinzani alishinda kwa sababu alinunua kura.

Pena Nieto anaingia madarakani akikabiliwa na jukumu kubwa la kuhakikisha anaendeleza vita ya kupambana na magenge ya wauzaji wa dawa za kulevya ambayo ilianzishwa na mtangulizi wake Felipe Calderon.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.