Pata taarifa kuu

Watu zaidi ya 230 wamefariki katika ajali ya treni nchini India

NAIROBI – Zaidi ya watu 230 wamefariki na wengine 900 kujeruhiwa katika ajali ya treni mashariki mwa jimbo la Odisha nchini India. Treni tatu zinaaminika kugongana katika ajali hiyo.

Hii ndio ajali mbaya zaidi ya treni kuwahi tokea nchini humo katika karne hii
Hii ndio ajali mbaya zaidi ya treni kuwahi tokea nchini humo katika karne hii REUTERS - STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Idadi ya waliofariki inatarajiwa kuongezeka katika kile kinachotajwa kuwa ajali mbaya zaidi ya treni kuwahi kutokea katika karne hii.

Zaidi ya magari 200 ya kubebea wagonjwa yalitumwa katika eneo la tukio katika wilaya ya Balasore, kwa mujibu katibu mkuu wa Odisha Pradeep Jena.Treni moja ya abiria inasemekana iliacha njia ya reli kabla ya kugongana na nyingine usiku wa Ijumaa.

Inahofiwa kuwa huenda idadi ya waliofariki katika ajali hiyo ikaongoza zaidi
Inahofiwa kuwa huenda idadi ya waliofariki katika ajali hiyo ikaongoza zaidi AP

Hii ndio ajali  mbaya zaidi ya treni nchini India katika karne hii. Maofisa wanasema idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka zaidi.

Shirika la Reli la India lilisema treni mbili zilizohusika katka ajali hiyo ni Coromandel Express na Howrah Superfast Express.

Hii ndio mojawapo ya ajali mbaya zaidi ya treni kuwahi tokeo nchini India katika karne hii
Hii ndio mojawapo ya ajali mbaya zaidi ya treni kuwahi tokeo nchini India katika karne hii AP

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi alisema amesikitishwa na tukio hilo na kutoa pole zake kwa familia zilizofiwa.

Naye waziri wa mambo ya ndani Amit Shah alitaja tukio hilo kuwa la "kuumiza sana". Siku ya maombolezo imetangazwa katika jimbo hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.