Pata taarifa kuu
URUSI

Balozi wa Marekani nchini Urusi kurudi Washington kwa Mashauriano

John Sullivan, balozi wa Marekani nchini Urusi, atarudi nchini Marekani wiki hii kwa mashauriano, kabla ya mkutano uliopangwa kati ya Marais Joe Biden na Vladimir Putin, shirika la habari la Ria limeripoti leo Jumanne.

Balozi wa Marekani nchini Urusi John Sullivan katika mkutano na waandishi wa habari huko Moscow, Urusi Januari 30, 2020.
Balozi wa Marekani nchini Urusi John Sullivan katika mkutano na waandishi wa habari huko Moscow, Urusi Januari 30, 2020. REUTERS - Evgenia Novozhenina
Matangazo ya kibiashara

Wiki iliyopita Urusi iliwafukuza wanadiplomasia 10 wa Marekani kwa kulipiza kisasi Washington baada ya hatua yake ya kuwafukuza wanadiplomasia 10 wa Urusi.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, wakati huo alipendekeza John Sullivan kurudi Washington kwa mashauriano, kulingana na shirika la habari la Interfax.

Washington wiki iliyopita ilitangaza kuwafukuza wanadiplomasia 10 wa Urusi na kuweka vikwazo mbali mbali dhidi ya Urusi, ikiishtumu Moscow kwa  kuingilia uchaguzi wa urais wa Marekani mwezi wa Novemba mwaka uliyopita, vitendo vya udukuzi wa kimtandao na  uhasama dhidi ya Ukraine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.