Pata taarifa kuu
GUATEMALA-MAANDAMANAO-USALAMA

Makao makuu ya Bunge yachomwa moto Guatemala

Maelfu ya watu wameandamana na kukusanyika kwa amani katika eneo kuu la Jiji la Guatemala (mji mkuu) Jumamosi, Novemba 21 wakipinga dhidi ya kupunguzwa kwa bajeti, hatua iliyochukuliwa na serikali.

Waandamanaji hao wametoa wito kwa rais Alejandro Giammattei kupinga bajeti hiyo iliyopitishwa Jumatano ya wiki hii.
Waandamanaji hao wametoa wito kwa rais Alejandro Giammattei kupinga bajeti hiyo iliyopitishwa Jumatano ya wiki hii. REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Kando na maandamano hayo, waandamanaji wengine wenye hasira walichoma moto makao makuu ya Bunge la nchi hiyo. Waandamanaji hao walikuwa wamebebelea bendera za nchi hiyo na mabango yaliyoandikwa "Giammattei, ajiuzulu".

Waandamanaji hao wametoa wito kwa rais Alejandro Giammattei kupinga bajeti hiyo iliyopitishwa Jumatano ya wiki hii.

"Bunge limetenga pesa zaidi kwa manufaa yake ikilinganishwa na pesa zilizotengwa kwa maskini," amesema Diego Herrera, mwanafunzi wa miaka 25, ambaye ni mmoja wa waandamanaji hao wenye hasira.

Hali ya sintofahamu inaendelea kuripotiwa katika miji mbalimbali ya Guatemala.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.