Nigeria - Usalama
Nigeria : Watu wanne wafariki baada ya mlipuko
Polisi nchini Nigeria wamesema zaidi ya watu wanne wamefaraiki baada ya kutokea kwa mlipuko karibu na shule moja ya msingi, ambayo pia paa zake zimaharibiwa, katika jimbo la Kano, kaskazini mwa taifa hilo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Uchunguzi wa mwanzo umeonyesha kuwa huenda mlipuko huo ulitokana na mtungi wa gesi, katika duka moja la choma vyuma, huko Sabon Gari.
Jimbo la Kano ni miongoni mwa majimbo ambayo yana idadi kubwa ya raia nchini Nigeria, na mlipuko huo umesabisha wasiwasi miongoni mwa raia kutokana na mashambulizi ya wanajihadi nchini Nigeria, ila jimbo hilo halijakuwa likishuhudia mashambulizi mara kwa mara.