Pata taarifa kuu
ETHIOPIA-USALAMA

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy arejea Addis Ababa kutoka uwanja wa vita

Waziri mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, amesema anarajea jijini Addis Ababa kutoka eneo la kaskazini mwa nchi hiyo, ambapo amekuwa akiongoza jeshi la nchi yake kupambana na waasi wa Tigray.  

Kiongozi wa Ethiopia Abiy Ahmed, ametangaza kurejea Ofisini baada ya jeshi la serikali mapema wiki hii kutangaza kupiga hatua kubwa katika uwanja wa vita.
Kiongozi wa Ethiopia Abiy Ahmed, ametangaza kurejea Ofisini baada ya jeshi la serikali mapema wiki hii kutangaza kupiga hatua kubwa katika uwanja wa vita. EDUARDO SOTERAS AFP/File
Matangazo ya kibiashara

Abiy Ahmed, mwezi Novemba, alikwenda kwenye mstari wa mbele  na kuacha madaraka kwa makamu wake kwa, baada ya waasi kuripoti kuchukua miji ya kimkakati na kusema wanaelekea jijini Assia Ababa.  

Kiongozi huyo wa Ethiopia, anarejea Ofisini baada ya jeshi la serikali mapema wiki hii, kutangaza kupiga hatua kubwa kwa kudhibiti miji ya kimkakati ya Dessie na Kombolcha kutoka kwa waasi.

Haya yanajiri wakati huu Mjumbe maalum wa Umoja wa Afrika katika Pembe ya Afrika Olusegun Obasanjo, akiendelea na jitihada za  kukomesha mapigano, lakini maendeleo madogo yameripotiwa kufikia sasa.

Mzozo huo unaozidi kukithiri, umechochea hofu ya uwezekano wa kusambaa katika eneo la Afrika Mashariki, huku Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mwezi uliopita, akizitaka pande zote mbili kuweka silaha chini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.