Serikali ya Ethiopia yataka waasi kujisalimisha na iko tayari kuwasamehe
Serikali ya Ethiopia inasema iko tayari kutoa msamaha kwa viongozi wa makundi ya waasi ili kupata amani ya kudumu , na kuwataka waeze kujisalimisha.
Imechapishwa:
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameendelea kuyashtumu mataifa ya Afrika kuendelea kutoa msamaha kwa waasi ambao wamehusika na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.
Mapigano kwenye mikoa ya Tigray, Amhara na Afra nchini Ethiopia, yameripotiwa kuanza kusambaa kwenye maeneo mengine ya taifa hilo, huku raia wakiuawa.
Hivi kaibuni Waziri Mkuu Abiy Ahmed kwa mara nyingine alitoa wito wa mshikamano wa kitaifa kukabili chama cha TPLF, ambacho, kwenye akaunti yake ya Twitter, alikiita "saratani".