Pata taarifa kuu
CHAD

Chad yawarejeha nyumbani wanajeshi 600 kutoka kikosi cha G5 Sahel

Chad imetangaza kwamba imeondoa nusu ya wanajeshi wake waliopelekwa mwezi Februari katika kikosi cha kupambana na wajihadi cha G5 Sahel katika eneo linaloitwa "mipaka mitatu", maeneo ya mpaka wa Mali, Niger na Burkina Faso.

Wanajeshi wa Chad walitumwa kama sehemu ya Kikosi cha Pamoja cha Jeshi dhidi ya Boko Haram, Nigeria.
Wanajeshi wa Chad walitumwa kama sehemu ya Kikosi cha Pamoja cha Jeshi dhidi ya Boko Haram, Nigeria. REUTERS/Emmanuel Braun
Matangazo ya kibiashara

Msemaji wa serikali ya Chad Abderaman Koulamallah, amesema idai hiyo haitzuia jitihada ya kikosi hicho kupambana na wanajihadi.

Kikosi hicho kilifika siku ya Alhamisi jioni katika nchini Chad baada ya zoezi la kuondoka lililoratibiwa na washirika wa G5 Sahel na Ufaransa vyanzo vya usalama kutoka Chad vimebaini.

Wanajeshi hao ni 600, nvimebaini vyanzo hivyo, ambavyo vimeongeza kuwa maelfu ya waasi wamekuwa wakitafuta kwa miezi kadhaa kurudi katika mji mkuu.

Kwa hivyo ni mbinu ya mkakati ambayo haitabadilisha chochote katika vita dhidi ya ugaidi huko Sahel, amesema msemaji wa serikali ya Chad, Abdéramane Koullamallah.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.