Sudan: idadi ya waliouawa Darfur Magharibi yaongezeka hadi 132
Hali sasa ni "tulivu" huko El-Geneina, mji mkuu wa Darfur Magharibi, unaokabiliwa na mapigano ya kikabila tangu Jumamosi. Mkuu wa mkoa huu unaopakana an Chad Mohamed abdalla Douma, ametangaza leo Alhamisi Aprili 8 kwamba idadi ya waliouawa sasa imefikia 132. Hakuna "mapigano tena" lakini "uporaji" unaendelea, ameongeza
Imechapishwa:
"Wanamgambo" walioushambulia mji huo walikuja wakitokea "nchi jirani kama vile Chad na Libya" na walitumia "silaha za kivita", amebaini Mohamed Abdallah Douma.
Mapigano hayo yalizuka wakati "kundi lenye silaha lilishambulia raia walipokuwa wakienda mjini", na kuua watatu, afisa huyo amesema. Umoja wa Mataifa, kwa upande wake, ulilikuwa umebaini "mapigano kati ya kabila la Al-Massalit na makabila ya Kiarabu".