Pata taarifa kuu
ETHIOPIA-USALAMA

Ethiopia / Tigray: Waziri Mkuu atangaza majibu makali baada ya shambulio dhidi ya kambi ya jeshi

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ametangaza kwamba chama cha Tigray People's Liberation Front (TPLF), chama tawala katika eneo hilo la Ethiopia, "kimeshambulia kambi ya jeshi la shirikisho," na Bwana Abiy ameagiza jeshi kuzima uasi huo.

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed. AFP/Monirul BHUIYAN
Matangazo ya kibiashara

Hatua ya setikali kuu ya Addis Ababa inaashiria uwezekano wa kuanza kwa mzozo nchini Ethiopia, nchi ya pili yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika, inayosumbuliwa na mivutano ya ndani.

"TPLF imeshambulia kambi ya kijeshi (shirikisho) huko Tigray. Imejaribu kuteka makao makuu ya jeshi ya Kaskazini," Abiy Ahmed amesema katika taarifa iliyorushwa kwenye Facebook na Twitter.

"Vikosi vyetu vya ulinzi vimepewa agizo (...) la kuchukua jukumu lake la kuokoa taifa. Hatua ya mwisho ya mstari mwekundu imevukwa. Kikosi kinatumika kwa kiwango sawa kuokoa raia na nchi, ”Bw;. Abiy ameongeza.

Haikuwezekana kupata maelezo zaidi juu ya shambulio hili linalodaiwa huko Tigray, ambalo wahusika hawakuweza kupatikana kwa simu kulingana na shirika la habari la REUTERS.

Vivyo hivyo, hali halisi ya jibu la kijeshi la shirikisho haikujulikana mara moja, lakini wachambuzi kadhaa na wanadiplomasia hivi karibuni wameelezea wasiwasi wao juu ya uwezekano wa kuzuka kwa mzozo kati ya kambi hizo mbili.

Mvutano umeongezeka siku za hivi karibuni kati ya Addis Ababa na mamlaka huko Tigray, ambayo haitambui tena mamlaka ya serikali ya shirikisho tangu uchaguzi wa kitaifa ambao uliotarajiwa kufanywa mwezi uliopita wa Agosti ambao uliahirishwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.