RSF: Tuna wasiwasi kuhusu uhuru wa Vyombo vya Habari Afrika
Wakati Ijumaa wiki hii dunia ikiadhimisha siku ya kimataifa ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, jumla ya waandishi wa habari 95 waliuawa mwaka uliopita na hii ni kwa mujibu wa shirikisho la kimataifa la wanahabari IFJ.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Siku hii inaadhimishwa huku dunia ikishuhudia waandishi wa habari wakiendelea kuuawa, kupokea vitisho, kuteswa , kupotezwa na hata kutekwa kwenye maeneo mbalimbali duniani.
Bara la Afrika ni miongoni mwa maeneo yanayotajwa kuwa hatari zaidi kwa waandishi wa habari kufanya kazi huku ikishuhudiwa vyombo vingi vikifungwa au kupokea vitisho.
Kwa upande wake shirika la waandishi wa habari wasio na mipaka RSF, lenyewe linaonya dhidi ya Serikali zinazominya uhuru wa habari, likitolea mfano hali inayoshuhudiwa nchini Burundi.