Pata taarifa kuu
ERITREA-ETHIOPIA-USHIRIKIANO

Rais wa Eritrea apongeza juhudi za Waziri Mkuu wa Ethiopia

Rais wa Eritrea Isaias Afwerki anasema nchi yake na Ethiopia, zimejengeana kuaminiana baada ya kutia saini mkataba mpya wa ushirikiano mwezi Julai.

Rais wa Eritrea Isaias Afwerki (kushoto) na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed (kulia).
Rais wa Eritrea Isaias Afwerki (kushoto) na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed (kulia). REUTERS/GHIDEON MUSA ARON VISAFRIC
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo, rais Afwerki amesema mataifa hayo mawili bado yanahitaji kusuluhisha baadhi ya mambo ili kuimarisha zaidi uhusiano huo mpya.

Eritrea na Ethiopia zilitiliana saini makumbaliano katika mkutano nchini Saudi Arabia ya kuboresha uhusiano baina ya nchi hizo mbili zilizowahi kuwa kwenye mvutano kwa miaka 20.

Mfalme wa Saudi Arabia, Salman bin Abdulaziz Al Saud (kati), Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed (kulia) na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki (kushoto).
Mfalme wa Saudi Arabia, Salman bin Abdulaziz Al Saud (kati), Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed (kulia) na Rais wa Eritrea Isaias Afwerki (kushoto). REUTERS/Saudi News Agency

Tangu mwaka 1998, matafa hayo yalianza kutofautiana kuhusu biashara na baadaye kulifuatia vita vya kuwania mpaka, vilivyosababisha vifo vya watu 80,000.

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed na Waziri Mkuu wa Eritrea Isaias Afwerki wakitia saini kwenye mkataba wa kusitisha miaka 20 ya vita Julai 9, 2018.
Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed na Waziri Mkuu wa Eritrea Isaias Afwerki wakitia saini kwenye mkataba wa kusitisha miaka 20 ya vita Julai 9, 2018. Twitter/Yemane G. Meskel
Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.