Chama tawala nchini Malawi chakutana kumchagua naibu kiongozi
Chama tawala nchini Malawi cha Democratic Progressive Party (DPP) kinafanya mkutano wake hivi leo ambao utamchagua Naibu Kiongozi kuchukua nafasi ya Saulos Chilima ambaye alitangaza kung'atuka mwezi uliopita.
Imechapishwa:
Kiongozi atakayechaguliwa huenda akawa mgombea mwenza wa rais Peter Mutharika katika uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Mei, mwakani.
Wakati wajumbe wa mkutano huo wakikutana Mjini Blantyre, gazeti la Nyasa Times limearifu katika toleo lake la leo kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo Dr. George Chaponda alianguka kabla ya kuhutubia wajumbe wa mkutano wa uchaguzi.
Wagombea wengine wa nafasi ya naibu rais ni Henry Mussa na Joseph Mwanamveka.
Chini ya mwaka mmoja kabla ya kufanyika kwa uchaguzi kumeripotiwa migawanyiko ndani ya chama tawala inayotajwa kusababishwa na makundi yanayojipanga kuwania uongozi katika uchaguzi ujao.
Ripoti ya Mwandishi wa RFI Kiswahili, Fredrick Nwaka