Mapigano yaibuka Sudani Kusini
Mapigano mapya yamezuka tena katika jimbo lenye utajiri wa mafuta la Unity nchini Sudan Kusini kati ya jeshi na waasi na zaidi ya watu thelathini wamepoteza maisha.
Imechapishwa:
Mapigano haya yamesabaisha mashirika ya Kimataifa ya kutoa huduma za kibiandamu kuondoka katika jimbo hilo.
Wakati huo huo waasi nchini Sudan Kusini wameitadharisha serikali ya nchi hiyo kwa kile wanachosema kuwa kuna dalili zinazoonyesha kuwepo dhamira ya kutaka ya kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoshiniwa hivi karibuni, hali ambayo wanasema inaweza kuirejesha nchi hiyo kwenye machafuko yaliyodumu muda wa miezi sihirni na moja sasa.
Kauli hii ya waasi inakuja baada yao kusema kuwa hawakufurahishwa na hatua ya rais Salva Kiir kuamuru kuongezwa kwa idadi ya majimbo kutoka 10 hadi ishirini na nane, hatua ambayo ilitangazwa na serikali siku ya Ijumaa iliyopita.
Waasi wamesema ikiwa mambo yatakuwa hivyo basi huenda kipengele kinachohusu mpango wa kugawana madaraka kuanzia ngazi za chini hadi serikalini kikavunjika.