Guinea watinga hatua ya fainali, michuano ya vijana
Time ya vijana ya Guinea Chini Ya Miaka 13 imefaulu Kucheza hatua ya fainali ya Michuano ya Afrika kwa vijana Chini ya Miaka 17 inayoendelea Jijini Dar es Salaam.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Timu Hiyo Kutoka Afrika Magharibi Imepata ushindi Wa mikwaju ya penati 10-9 baada ya Timu Hizo Kutoka Sare ya Bila kufungana Katika dakika 90 za mchezo.
Kwa Matokeo hayo Guinea itachuana na mshindi baina ya Cameroon na Angola ambazo pia zimekuwa zikichuana jana.
Mwandishi Wa RFI Kiswahil, Fedrick Nwaka aliyeshuhudia Mchezo huo, anasema Nigeria Licha ya Kupewa Nafasi Kubwa ilishindwa Kufua dafu.
Licha ya Kupoteza mchezo huo Nigeria, Sanjari Na Angola, Guinea na Cameroon Zitawakilisha bara la Afrika Katika Fainali za vijana zitakazochezwa Baadaye Mwaka huu Nchini Brazil.