CHAN 2018: Morocco yaiadhibu Nigeria 4-0
Morocco iliifunga Nigeria mabao 4-0 na kuibuka washindi katika michuano ya kombe la Afrika kwa wachezaji wa Ligi za ndani ( CHAN), mchezo uliopigwa jana Jumapili.
Imechapishwa:
Wenyeji Morocco walifanikiwa kulinyanyua taji la michuano hiyo kufuatia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Nigeria.
Bao la kwanza la Morocco lilipachikwa wavuni na Zakaria Hadraf muda mfupi baada ya kuanza kipinzi cha pili.
Dakika mbili baada ya kipindi cha mpumziko Peter Eneji Moses alitimuliwa uwanjani baada ya kupewa kadi ya pili ya njano kwa mchezo m'baya dhidi ya Mohammed Nahiri.
Bao la pili la Nigeria lilifungwa na Walid El Karti, huku Hadraf akipachika bao la tatu
Ayoub El Kaabi alikamilisha mchezo huo kwa kufunga bao la nne na hivyo kupelekea Morocco kutwaa taji la ichuano hiyo.