May: Mswada wa kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya kuwekwa wazi mwezi Juni
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amesema mswada wa nchi hiyo kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya, hautajadiliwa au kuchapishwa hadi mapema mwezi Juni.
Imechapishwa:
May ametoa kauli hii wakati huu anapoendelea kupata shinikizo, ajiuzulu baada ya kuahidi kuwa ataleta mswada mpya.
Hii inakuja baada ya mmoja wa Waziri Andrea Leadsom, kujiuzulu Jumatano usiku kuhusu mpango mpya wa Waziri May.
Waziri Mkuu May, siku ya Jumatano, aliwaambia wabunge wana nafasi ya mwisho kuamua mustakabali wa nchi hiyo kujiondoa kwenye umoja huo au waamue kuwa na kura nyingine ya maoni.
Uingereza imepewa hadi mwisho wa mwezi Oktoba kupitisha mswada wa kujiondoa kwenye Umoja huo.