Pata taarifa kuu
UFARANSA-UN-HAKI

Vizibao vya Njano: UN yaomba uchunguzi kuhusu "matumizi ya nguvu za kupita kiasi

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeitaka Ufaransa "kufanya uchunguzi wa kina" kuhusu machafuko ya polisi wakati wa maandamano ya "vizibao vya njano" tangu mwanzoni mwa mwezi Novemba mwaka jana.

Vikosi vya usalama vya Ufaransa, wakitumia LBD wakati wa "maandamano ya tano" ya "vizibao vya njano", Desemba 15  Paris.
Vikosi vya usalama vya Ufaransa, wakitumia LBD wakati wa "maandamano ya tano" ya "vizibao vya njano", Desemba 15 Paris. Valery HACHE / AFP
Matangazo ya kibiashara

Katika hotuba ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu mjini Geneva, Michelle Bachelet amesema kuwa "vizibao vya njano" wanaandamana dhidi ya "kile wanachoona kama kutengwa kwa haki za kiuchumi na kushiriki katika masuala ya umma ".

"Tunaiohimiza Serikali kuendelea na mazungumzo na tunaomba kufanya haraka uchunguzi wa kina kuhusu kesi zote zinazohusiana na matumizi ya nguvu za kupota kiasi," ameongeza Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu.

Michelle Bachelet amekumbusha kuwa "nchi karibu zote zinakumbwa na suala ka kutofautiana" na hata "katika nchizilizostawi kiuchumi, watu wanajihisi kuwa wametengwa kwa faida za maendeleo na kunyimwa haki za kiuchumi na kijamii".

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.