BEMBA-DRC-UBELGIJI-ICC
Ubelgiji yakubali kumpa makaazi Bemba
Ubelgiji imesema iko tayari kumpokea na kumpa makaazi Jean Pierre Bemba, aliyekuwa Makamu wa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya Mahakama ya Kimataifa ya ICC, kumwachilia huru wiki hii.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Waziri wa Mambo ya nje wa nchi hiyo Didier Reynders amesema utaratibu unaendelea,ili kumruhusu Bemba kuungana na familia yake inayoishi katika taifa hilo la bara Ulaya.
Bemba, ameomba kuishi nchini Ubelgiji kwa muda wa miezi mitatu na tayari ameomba kibali.
Haijafamika iwapo atarejea nchini DRC na labda kuwania urais mwezi Desemba.
Bonyeza hapa kusoma zaidi kuhusu Bemba:-