Edouard Philippe: Sheria mpya ya kazi itatekelezwa kikamilifu
Waziri Mkuu wa Ufaransa Edouard Philippe amesema Serikali ya nchi hiyo iko imara na itahakikisha sheria mpya ya kazi inatekelezwa kikamilifu.
Imechapishwa:
Waziri Mkuu wa Ufaransa Edouard Philippe amesema Serikali iko imara na itahakikisha sheria ya kazi inatekelezwa katika nchi hiyo.
Akiandamana na waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa katika mji wa Bourges.
Waziri mkuu Philippe amelaani maandamano ya wafanyakazi yaliyofanyika mei mosi mjini Paris.
Waziri huyo amesema rubani yuko ndani ya ndege na kila kitu kinaenda vizuri, akimaanisha rais Emmanuel Macron anashikilia usukani, kauli ambayo aliitoa katika kuwakemea wapinzani wa serikali wanaokosoa serikali yake.