Pata taarifa kuu
G7-SYRIA

Mawaziri wa G7 washindwa kukubaliana kuhusu vikwazo vipya dhidi ya Syria na Urusi

Mawaziri wa mambo ya kigeni kutoka nchi zilizoendelea kiviwanda G7 wameshindwa kukubaliana kuhusu kutangaza vikwazo vipya dhidi ya rais wa Syria Bashar al-Assad au mshirika wake nchi ya Urusi, amesema waziri wa mambo ya nje wa Itali Angelino Alfano.

Waziri wa mambo ya nje wa Italia Angelino Alfano akizungumza wakati wa mkutano wa nchi za G7. April 11, 2017.
Waziri wa mambo ya nje wa Italia Angelino Alfano akizungumza wakati wa mkutano wa nchi za G7. April 11, 2017. REUTERS/Max Rossi
Matangazo ya kibiashara

Waziri Alfano amesema kuwa "kwa wakati huu hakuna muafaka kuhusu vikwazo vipya kama njia sahihi," amesema wakati wa mkutano wa siri wa siku mbili nchini Italia, baada ya waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza Boris Johnson kuibua suala hilo kwenye mkutano wao.

"Hakuna mawazo ya wazi yaliyotofauti," amesema Alfani ambaye ameongeza kuwa nchi za G7 zimesisitiza uungaji mkono wao kuhusu vikwazo ambavyo vimewekwa kwa sasa.

Jumatatu ya wiki hii waziri Johnson aliibua suala la kutangaza vikwazo zaidi kwa baadhi ya maofisa wa juu wa jeshi la Syria na wale wa Urusi ambao wamekuwa wakishiriki kuratibu operesheni za kijeshi.

Waziri wa fedha wa Marekani Steven Mnuchin alisema wiki iliyopita kuwa Marekani hivi karibuni itatangaza vikwazo zaidi kwa nchi ya Syria kama sehemu ya kijeshi, dipolomasia na ufadhili wa fedha baada ya shambulio la silaha za kemikali.

Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Marc Ayraut amethibitisha waziri Johnson kuwasilisha wazo hilo hata asubuhu ya Jumanne lakini nchi washirika hazikulijadili suala hilo kwa kina.

Italia inasema inaamini vikwazo ni kama chombo na sio kumaliza tatizo lililopo na kuonya kuhusu hatua ambazo zitaitenga zaidi Urusi.

Katika hatua nyingine waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson amesema rais Bashar al-Assad hapaswi kuwa sehemu ya mustakabali ujao wa Syria.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.