Pata taarifa kuu
SERBIA-WAHAMIAJI-USALAMA

Wahamiaji wanaozuiliwa Serbia watafuta barabara nyingine

Mamia ya wahamiaji wamekwama katika mpaka wa Serbia na Hungary huku wakilazimika kulala nje kwenye kibaridi kikali kutokana na mpaka wa hungary kufungwa.

Wahamiaji wa Septemba 15, 2015 katika mji wa Horgos nchini Serbia karibu na mpaka na Hungary.
Wahamiaji wa Septemba 15, 2015 katika mji wa Horgos nchini Serbia karibu na mpaka na Hungary. Photo par ELVIS BARUKCIC/AFP
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema kuwa wahamiaji hao wengi wao kutoka nchini Syria wameanza kutafuta njia nyingine ya kwenda katika mataifa mengine ya Ulaya.

Hungary imeweka uzio kuwazuia wahamiaji hao lakini pia kupitisha sheria za kuwazuia wahamiaji kuingia katika ardhi yao.

Zoltan Kovac, msemaji wa serikali hiyo amesema wahamiaji ambao wanaweza kuruhusiwa ni wale waliokubaliwa rasmi kuingia nchini humo kupewa hifadhi ya kisiasa.

Austria pia imetangaza kudhibiti mipaka yake kuwazuia wahamiaji hao kuingia wengi wao wakiwa na lengo la kufika Ujerumani.

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel ameitisha mkutano wa dharura kuzungumzia wimbi hili la wahamiaji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.