Pata taarifa kuu

Urusi kuendelea kuwa tayari kutumia silaha za nyukilia: Rais Putin

Rais wa Urusi Vladimir Putin, kwa mara nyengine amesema nchi yake itaendelea kuwa tayari kutumia silaha zake za nyukilia na kwamba Moscow haitovumilia vitisho vyovyote kutoka kwa nchi za Magharibi.

Rais Putin ameendelea kusisitiza kuwa, vita vya sasa vinayoendelea nchini Ukraine ni vita vya dhidi ya utawala wa kinazi
Rais Putin ameendelea kusisitiza kuwa, vita vya sasa vinayoendelea nchini Ukraine ni vita vya dhidi ya utawala wa kinazi © via REUTERS - SPUTNIK
Matangazo ya kibiashara

Aidha, amewapongeza wanajeshi wake wanaopigana Ukraine ambapo amezituhumu nchi za Magharibi kwa kuchangia katika mizozo inayoshuhudiwa duniani.

Akizungumza wakati wa gwaride ya kuadhimisha siku ya ushindi wa nchi yake dhidi ya Ujerumani wakati wa vita vya pili vya dunia, Putin amewakumbusha raia wa nchi yake kuwa, wanakabiliwa na kipindi kigumu ambacho watashinda.

Rais Putin ameendelea kusisitiza kuwa, vita vya sasa vinayoendelea nchini Ukraine ni vita vya dhidi ya utawala wa kinazi.

Rais Putin ambaye aliapishwa wiki hii sasa atawaongoza raia wa Urusi kwa kipindi cha miaka sita.
Rais Putin ambaye aliapishwa wiki hii sasa atawaongoza raia wa Urusi kwa kipindi cha miaka sita. via REUTERS - Kremlin.ru

Mapema wiki hii, rais Putin aliviagiza vikosi vya nchi yake kwa ushirikiano na wanajeshi wa maji walio kwenye mpaka na nchi ya Ukraine kufanya mazoezi ya silaha za nyukilia.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo, vilitangaza kuwa gwaride hilo lingehudhuriwa na viongozi kutoka nchi nane ambazo ni washirika wa karibu wa Urusi.

Baadhi ya viongozi hao ni pamoja na wale kutoka katika nchi za Belarus, Kazakhstan, Kyrgyzstan, Tajikistan na Turkmenistan, pamoja na Cuba, Laos na Guinea-Bissau, mataifa ambayo Kremlin inasema ni rafiki zake.

Urusi imekuwa ikisisitiza kuwa vita vinavyoendelea nchini Ukraine vimechochewa na nchi za Magharibi.
Urusi imekuwa ikisisitiza kuwa vita vinavyoendelea nchini Ukraine vimechochewa na nchi za Magharibi. © Libkos / АР

Hotuba ya rais Putin imekuja wakati huu wanajeshi wa nchi yake wakiripotiwa kuendelea kupiga hatua katika uwanja wa vita nchini Ukraine.

Putin mwenye umri wa miaka 71, wiki hii ameapishwa tena kuiongoza nchi yake kwa kipindi kingine cha miaka sita baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa mwezi Machi ambao hata hivyo ulisusiwa na upinzani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.