Pata taarifa kuu

Urusi kuzipa nafaka nchi sita za bara Afrika

Nairobi – Rais wa Urusi Vladimir Putin ametangaza mpango wa kuzipa nchi sita maskini za bara Afrika nafaka bila malipo, tangazo la Putin likija siku chache baada ya nchi yake kujiondoa kwenye mkataba wa usafirishaji wa nafaka na Ukraine.

Mkutano wa Afrika na Urusi unafanyika mjini St Petersburg
Mkutano wa Afrika na Urusi unafanyika mjini St Petersburg AP - Pavel Bednyakov
Matangazo ya kibiashara

Wiki iliyopita, Moscow ilikataa kuongeza muda wa mkataba huo ambao ulikuwa unatoa nafasi kwa nchi ya Ukraine kusafirisha nafaka yake kupitia kwenye bahari nyeusi kwenda masoko ya kimataifa ikiwemo Afrika.

Wakati akihutubia mkutano wa bara Afrika na Urusi, rais Putin ameahidi kutuma nafaka kwa mataifa sita ya bara Afrika katika kipindi cha miezi michache ijayo.

Mkataba huo ulikuwa unaruhusu usafirishaji wa nafaka kupitia kwenye bahari nyeusi
Mkataba huo ulikuwa unaruhusu usafirishaji wa nafaka kupitia kwenye bahari nyeusi AP - Darko Vojinovic

Nchi ambazo zitanufaika na mpango huo wa Urusi ni pamoja na Burkina Faso, Zimbabwe, Mali, Somalia, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Eritrea.

Putin amesema nchi yake imepanga kuzipa nchi hizo kati ya tani 25,000 hadi tani elfu 50,000 za nafaka.

Mkataba huo ulikuwa unaruhusu usafirishaji wa karibia tani milioni 33 za nafaka kutoka katika bandari za nchini Ukraine na kusaidia katika kukabiliana na uhaba wa chakula.

Rais wa Afrika kusini ameonekana kuwa mshirika wa karibu wa rais wa Urusi barani Afrika
Rais wa Afrika kusini ameonekana kuwa mshirika wa karibu wa rais wa Urusi barani Afrika via REUTERS - JAIRUS MMUTLE/GCIS

Viongozi 17 kutoka katika mataifa ya bara Afrika akiwemo rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo wa siku mbili.

Kremlin imezituhumu nchi za Magharibi kwa kujaribu kuyazua mataifa ya Afrika kuhudhuria kongamano hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.