Ruto aidhinishwa kuwania kiti cha urais Kenya
Nchini Kenya, Tume ya Uchaguzi imemwidhinisha Naibu rais William Ruto kugombea urais wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Baada ya hatua hiyo, Ruto ambaye wiki hii alilalamika kuwa wapiga kura karibu Milioni moja kutoka kwenye ngome zake wameondolewa kwenye daftari la kupigia kura, amesema ana imani na Tume hiyo na baadaye akaongoza kampeni ya siasa jijini Nairobi.
Mgombea mwingine, Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga, anatarajiwa kuidhinishwa hapo kesho.
Ruto na Odinga, ndio wagombea wakuu wa Uchaguzi wa urais nchini Kenya.