UFARANSA
Karim Benzema apatikana na virusi vya Corona
Mshambuliaji Mfaransa Karim Benzema amefanyiwa vipimo na kukutwa na virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19, kilabu chake, Real Madrid, kimetangaza Ijumaa katika taarifa ya sauti bila maelezo zaidi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Karim Benzema alishiriki mnamo Juni michuano ya soka ya Ulaya katika timu ya taifa ya Ufaransa, iliyoondolewa na Uswisi katika raundi ya 16. Alifunga mabao manne wakati wa michuano hiyo.
Karim Benzema mwenye umri wa miaka 33, raia wa Ufaransa, alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Juni mwaka jana wa Ligi kuu nchini Uhispania maarufu kama LaLiga.