Jaji wa Mahakama nchini Serbia athibitisha kuwa Ratko Mladic yuko katika hali nzuri
Mahakama nchini Serbia imesema kuwa Jenerali wa zamani wa Bosnia Ratko Mladic yuko katika hali nzuri kusimama mbele ya mahakama ya kimataifa ya UN kulingana na uamuzi uliotolewa na jaji Maja Kovacevic, na sasa atafika mbele ya mahakma ya umoja wa mataifa kwa tuhuma za mauji ya kimbari nchini humo mwaka 1995.Mladic alikamatwa jana namaafisa wa usalama wa Serbia, swala ambalo limeungwa mkono na jamii ya mataifa, na kiongozi wa mashtaka nchini humo amesema kuwa ni sharti Mladic afikishwe mahakamani na kufunguliwa mashataka, kama anavyoleza Bruno Vekaric.
Imechapishwa:
Cheza - 00:33
Hapo awali,mwanawe Mladic,Darko Mladic alisema kuwa babake alikuwa katika hali mbaya ya kiafya ambayo haingemruhusu kushtakiwa.