Pata taarifa kuu

Kombe la Dunia la Soka 2023: Morocco yapata ushindi wa kihistoria dhidi ya Korea Kusini

Baada ya kushindwa dhidi ya Ujerumani (6-0), Morocco, ambayo inashiriki kwa mara ya kwanza michuano ya Kombe la Dunia la Wanawake, imepata ushindi wa kihistoria dhidi ya Korea Kusini  kwa kuifunga bao 1-0 huko Adelaide, nchini Australia.

Kikosi cha wachezaji wanawake wa Morocco wakishangilia ushindi wao dhidi ya Korea Kusini.
Kikosi cha wachezaji wanawake wa Morocco wakishangilia ushindi wao dhidi ya Korea Kusini. © Hannah Mckay, Reuters
Matangazo ya kibiashara

Morocco, haikufikiriwa kuwa itafanya vizuri katika mashindano hayo, imepata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano hii ya Kombe la Dunia la Wanawake, dhidi ya Korea Kusini (1-0), Jumapili Julai 30, huko Adelaide, kwa bao la kichwa lililowekwa kimyani na Ibtissam Jraidi dakika ya 6 ya mchezo.

Wachezaji hao wanaonolewa soka na kocha Reynald Pedros, waliochapwa na Ujerumani (6-0) walipoingia kwenye kinyang'anyiro hicho, wamesalia kwenye kinyang'anyiro cha kufuzu kwa hatua ya 16 bora, kabla ya kumenyana na Colombia siku ya mwisho ya kundi H, Alhamisi, Agosti 3.

(Pamoja na AFP)

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.