IRAQ-IS-SHAMBULIO
Iraq: helikopta ya jeshi yaangushwa na IS
Kundi la Islamic State (IS) limeiangusha helikopta ya jeshi la Iraq magharibi mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad, na kuua mwanajeshi mmoja, maafisa wamesema.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Tukio hili limetokea Jumatano hii, Februari 17, 2017.
Helikopta hii ambayo ni ya pili Iraq inapoteza kwa muda wa siku mbilia imeangushwa karibu na mji wa Amriyat al-Fallujah. Hata hivyo maafisa bado wanatofautiana juu ya eneo halisi ambapo helikopta hiyo imedunguliwa.