New Zealand
Meli iliovuja mafuta nchini New Zealand yaendelea kuchafuwa bahari
Serikali ya New Zealand inaendelea kusafisha eneo la bahari yake ambalo limechafuliwa kutokana na kuvuja kwa mafuta kutoka katika meli moja licha ya yenyewe kukiri kazi hiyo itakuwa ni ngumu.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wataalam wa Masuala ya Bahari nchini New Zealand wanaendelea na kibarua hicho huku wakisema itachukua muda kidogo ili kurejesha hali kama ilivyokuwa awali kwani mafuta hayo yamechafua eneo kubwa.
Waziri Mkuu wa New Zealand John Key amesema wanaendelea na juhudi za kuhakikisha wanadhibiti uchafuzi huo wa bahari ambao umejitokeza lakini watakuwa makini kwenye kutekeleza hilo.