Rais George Weah akubali kushindwa kwenye duru ya pili ya uchaguzi
Imechapishwa:
Cheza - 20:03
Matukio kadhaa wa kadhaa yamefanyika ulimwenguni kukiwemo George Weah kukubali kushindwa katika duru ya pili ya uchaguzi nchini Liberia kwa Joseph Boakai. Hii ina maana atakuwa miongoni mwa marais waliohudumu kwa muhula mmoja.
Tutaangazia pia mafuriko yalivyoathiri nchi nyingi, Hali ya usalama na kisiasa nchini DRC, kadhalika Kenya kuidhinisha polisi kutumwa Haiti, tutaangazia uamuzi wa mahakama ya Uingereza kuhusu sera ya wahamiaji nchini Rwanda, kadhalika usalama Mali na chaguzi nchini Madagascar na hali halisi katika vita vinavyoendelea huko Gaza na pia tutaangazia mkutano kati ya Rais Joe Biden na Xi Jinping.