Ujumbe wa viongozi wa bara Afrika wanaojaribu kuzishawishi nchi za Urusi na Ukraine kumaliza mapigano yanayoendelea unatarajiwa kuzuru Moscow na Kiev kuanzia mwezi ujao.
Matangazo ya kibiashara
Taarifa hii imethibitishwa na ofisa wa ngazi ya juu katika serikali ya Afrika Kusini, nchi ambayo imeonekana kuwa mshirika wa karibu wa rais Putin.
Marais za Zambia, Senegal, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda, Misri na Afrika Kusini, wanatarajiwa kuongoza juhudi hizo, suala ambalo limekaribishwa na umoja wa mataifa.
Nini maoni yako kuhusu hatua hii? skiza makala haya