RDC: Waziri Mkuu Jean-Michel Sama Lukonde, amejiuzulu
Nairobi – Waziri mkuu wa nchi ya DRC, Jean-Michel Sama Lukonde, amejiuzulu nafasi yake hapo jana, uamuzi unaomaanisha kuvunjwa kwa Serikali yake, ikulu ya Kinshasa imethibitisha, hata hivyo bila kueleza sababu za kufanya hivyo.
Imechapishwa:
Cheza - 01:05
Hatua ya kujiuzulu kwake inakuja baada ya Muda wa siku 8 uliokuwa umetolewa kwa wajumbe wa Serikali waliochaguliwa kuwa wabunge wa bunge la taifa nchini humo kumalizika Jumanne Februari 20 saa sita usiku.
Lukonde amechagua kushiriki vikao vya Bunge kwa mujibu wa matakwa ya Ibara ya 108 ya Katiba inayowataka viongozi waliochaguliwa kuchagua kati ya kazi zao serikalini na kuwawakilisha wananchi.
#RDC 20.02.2024|#CiteUA
— Présidence RDC 🇨🇩 (@Presidence_RDC) February 20, 2024
Le Premier ministre @LukondeSama vient de déposer sa démission auprès du Président Félix Tshisekedi. Il était à la tête du Gouvernement depuis le 15 février 2021, au terme des consultations nationales que le Chef de l’État avait initiées en novembre 2020. pic.twitter.com/66QP8qo87a
Awali, baadhi ya waliokuwa mawaziri wa timu yake nao waliwasilisha barua za kujiuzulu kwa rais miongoni mwao Vital Kamerhe (naibu Waziri Mkuu wa Uchumi), Jean-Pierre Lihau, Antipas Mbusa (Waziri anayesimamia Ushirikiano wa Kikanda) Julien Paluku kama Waziri wa Viwanda na wengine.
Sama Lukonde aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu mnamo Februari 15, 2021, mwishoni mwa mashauriano ya kitaifa ambayo rais Tshisekedi aliyaanzisha Novemba 2020, hata hivyo akiwataka baadhi kusalia hadi pale atakapoteua serikali mpya.