UCHUMI-MAZINGIRA
Total-Uganda: Tumetumia kila mbinu kuhakikisha kuwa mazingira na wanyamapori wanalindwa
Kampuni ya mafuta ya Ufaransa ya Total nchini Uganda, imesema mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima kwenda Tanga nchini Tanzania, imetumia kila mbinu kuhakikisha kuwa mazingira na wanyamapori wanalindwa.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kauli hii inakuja baada ya wabunge wa bunge la Umoja wa Ulaya, kupitisha azimio la kupinga kuendelea kwa mradi huo kwa madai kuwa, utaharibu mazingira.
Naye Balozi wa China nchini Uganda, Zhang Lizhong amelaani hatua hiyo ya wabunge wa Umoja wa Ulaya.
Kampuni ya China CNOOC inashirikiana na kampuni ya Total katika mradi huo wa bomba la mafuta.