Kenya - Siasa
Kenya : William Ruto kifua mbele - utafiti wa Intel Reserch Solution
Utafiti mpya wa kura ya maoni nchini Kenya, umeonesha kuwa naibu rais wa taifa hilo William Ruto, angelichaguliwa kwa asilimia 50.5 dhidi ya upinzani wake wa karibu waziri mkuu wa zamani Raila Odinga ambaye angepata asilimia 44.2 ya kura, iwapo uchaguzi ungeandaliwa leo nchini Kenya.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Cheza - 04:02
Matangazo ya kibiashara
Wagombe wengine George Wajakoya na David Mwaure wangepata asilimia 1.9 na 1.1 mtawalia.
Benson Wakoli amepata nafasi ya kuzungumza na afisa mkuu mtendaji wa shirika la Intel Reserch Solution ambalo limechapisha kura hii ya maoni na ameanza kwa kumuliza Karen Mwangi, anazungumzia utafiti huu.