CHINA-SYRIA
China yaahidi ushirikiano kwa mjumbe mpya wa umoja wa mataifa katika mzozo wa Syria.
China imepongeza umoja wa mataifa kwa kumchagua Lakhdar Brahimi kuwa mjumbe wa umoja huo katika mzozo wa Syria na kuahidi kushirikiana naye katika kutafuta suluhu ya mzozo huo.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Jana Ijumaa Umoja wa Mataifa umemtangaza mwanadiplomasia mkongwe kutoka nchini Algeria Lakhdar Brahimi kuwa mjumbe wa umoja huo akichukua nafasi ya Kofi Annan, ambaye alijiondoa mapema mwezi huu.
Katika maoni yake ya kwanza, Brahimi amekiri kutokuwa na ujasiri katika kumaliza mgogoro huo wa uliodumu kwa miezi 17 sasa.