Viongozi wa mataifa 7 yalioendelea kiucumi kukutana ijumaa Septemba 9 nchini Ufaransa
Viongozi kutoka mataifa tajiri duniani maarufu kama G7 wanatarajiwa kukutana hiyo kesho nchini Ufaransa kujadili kwa kina namna ya kumaliza matatizo ya kiuchumi ambayo yanashuhudiwa Barani Ulaya kwa sasa.
Imechapishwa:
Viongozi kutoka nchi za Marekani, Canada, Japan, Ujerumani, Uingereza, Ufaransa na Italia wanatarajiwa kuangalia ni kwa nini masoko ya hisa yameendelea kuyumba na kutishia hata usalama wa uchumi wa dunia.
Mkuu wa Shirika la Fedha Duniani IMF christine Lagarde ni miongoni mwa wale ambao watahudhuria mkutano huo muhimu kwa maendeleo na uchumi wa dunai ambao kwa sasa upo mashakani tangu Marekani ikimbwe na mgogoro wa kiuchumi.