Pata taarifa kuu

Senegal: AU yampongeza rais mteule Bassirou Diomaye Faye

Nairobi – Umoja wa Afrika, umempongeza rais mteule wa Senegal Bassirou Diomaye Faye ambaye alikuwa mgombea wa upinzani kwa ushindi wake katika uchaguzi mkuu wa urais.

Faye, 44, aliachiwa kutoka gerezani siku kumi kuelekea tarehe ya uchaguzi huo akiwa na kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko.
Faye, 44, aliachiwa kutoka gerezani siku kumi kuelekea tarehe ya uchaguzi huo akiwa na kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko. AFP - JOHN WESSELS
Matangazo ya kibiashara

Katika taarifa yake, Tume ya Umoja wa Afrika kupitia mwenyekiti wake Moussa Faki Mahamat imemtakia Faye mema katika nafasi yake mpaya.

Kwa mujibu wa matokeo ya awali, Faye aliibuka mshindi wa uchaguzi huo katika duru ya kwanza kwa kupata asilimia 54.3 dhidi ya mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na rais Macky Sall, waziri mkuu wa zamani Amadou Ba.

Mahakama ya katiba nchini Senegal inatarajiwa kumtangaza rasimi Faye kuwa mshindi wa uchaguzi huo kabla ya wikendi hii.

Faye, 44, aliachiwa kutoka gerezani siku kumi kuelekea tarehe ya uchaguzi huo akiwa na kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko, ambaye naye alizuiwa kugombea katika uchaguzi huo kutokana na mashataka ambayo alisema yalichochewa kisiasa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.