Kenya : Tamasha la wanahabari Africa
NAIROBI – Taasisi ya Baraza Media Lab nchini Kenya, inajiandaa kuwa mwenyeji wa awamu ya pili ya tamasha la wanahabari barani Africa, tamasha litakalofanyika mwezi huu tarehe 21 na 22, hafla itakayofanyika katika kituo cha makumbusho ya kitaifa jijini Nairobi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Zaidi ya wanahabari 300 wanatarajiwa kongamana jijini Nairobi kuhudhuri tamasha la mwaka huu kutoka mataifa 18 ya Africa, lengo likiwa kuwaleta pamoja wadau mbali mbali kujadili hali ya baadaye ya wanahabari barani , ambapo changamoto na mafanikio ya wanahabari wa Africa yatajadiliwa kwenye tamasha hilo la siku mbili.
Kwa mjibu wa Christine Mungai, mmoja wa waandalizi wakuu wa hafla hii, ni kwamba wanalenga kuwakutanisha wanahabari kutoka kote barani Africa ambapo watakutana na kujadili maswala mbalimbali ambayo huwaandama katika shughuli zao za kila siku.
CHRISTINE MUNGAI
Aidha imebainika kwamba huenda tamasha zitakazofuata zikandaliwa katika mataifa mengine ya Africa, baada ya nchi ya Rwanda kuonesha nia ya kutaka kuwa mwenyeji wa tamasha hilo.
Mbali na wanahabari patawepo pia watatumbuizaji kutoka kwa wacheshi wanamuziki.