Pata taarifa kuu

Kenya: Ruto atambuliwa kwa mchango wake kuhusu mazingira

Nairobi – Rais wa Kenya William Ruto ametambuliwa na Jarida la Time kuwa miongoni wa viongozi 100 wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani kutokana na mchangao wao kuhusu kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa duniani.

Wiki hii, Rais Ruto aliwaongoza raia wa taifa lake katika zoezi la upanzi wa miche  milioni 100 kwa siku moja.
Wiki hii, Rais Ruto aliwaongoza raia wa taifa lake katika zoezi la upanzi wa miche  milioni 100 kwa siku moja. AFP - LUIS TATO
Matangazo ya kibiashara

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya rais Ruto kuwaongoza raia wa taifa lake katika zoezi la upanzi wa miche  milioni 100 kwa siku moja.

Ruto aliteuliwa pamoja na meya wa mji mkuu wa Sierra Leone Freetown, Yvonne Aki-Sawyerr.

Mbunifu mwenye uraia wa Burkina Faso na  Ujerumani Francis Kéré na mjasiriamali wa hali ya hewa raia wa Ethiopia Kidus Asfaw pia walitambuliwa.

Rais Ruto amekuwa akitaka mataifa tajiri yanayoongoza kwa uchafuzi wa mazingira kuwajibishwa
Rais Ruto amekuwa akitaka mataifa tajiri yanayoongoza kwa uchafuzi wa mazingira kuwajibishwa AFP - LUIS TATO

Orodha hiyo, inayojulikana kama "Time 100 Climate", ilitolewa siku ya Alhamisi, na ni jaribio la uzinduzi wa jarida hilo kutaja wale inaowaona kuwa muhimu katika kuangazia na kufanya jambo kuhusu suala la mabadiliko ya hali ya hewa kote ulimwenguni.

Kwa mujibu wa Time, hatua hiyo iliafikiwa baada ya kuangazia juhudi na maendeleo  makubwa yaliopigwa katika kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Raia wa Kenya akipanda mgomba wa ndizi kando ya nyumba yake jijini Nairobi. Serikali imetoa nafasi wa raia wote kushiriki zoezi la upanzi wa miti
Raia wa Kenya akipanda mgomba wa ndizi kando ya nyumba yake jijini Nairobi. Serikali imetoa nafasi wa raia wote kushiriki zoezi la upanzi wa miti AP - Sayyid Abdul Azim

Jarida hilo pia lilisema kuwa viongozi hao walichaguliwa kwa sababu ya juhudi zao katika kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa ambayo yalikuwa ya hivi karibuni ambapo pia yalitoa mafanikio makubwa yanayoonekana.

Ruto amekuwa amekuwa mstari wa mbele kujaribu kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa nchini Kenya na Afrika.

Siku iliyotengwa na serikali kwa lengo la kupanda miche ambayo ilifanyika tarehe 13 Novemba ilikuwa sehemu ya azma yake kubwa kwa Kenya kupanda miti bilioni 15 katika miaka 10.

Wanafunzi na maofisa wa umma wanaongoza shughuli hiyo
Hatua hii imetajwa kuwa njia moja ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa AP - Sayyid Abdul Azim

Mnamo Septemba, aliandaa mkutano wa kwanza kabisa wa hali ya hewa barani Afrika katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, ambao ulimalizika kwa tamko la pamoja la kutaka mataifa yanayoongoza katika uchafuzi wa mazingira duniani kutoa rasilimali zaidi kusaidia mataifa maskini.

Licha ya hayo, aadhi ya wanamazingira wamemtaja rais Ruto kuwa mnafiki kwa kutetea upandaji miti huku akikosa kudhibiti ukataji miti ovyo katika misitu ya umma.

Zoezi linaoongozwa na rais William Ruto
Raia wa Kenya wakipanda miche jijini Nairobi AP - Sayyid Abdul Azim

Mwezi uliopita, mahakama ya mazingira ilisitisha agizo ambalo Ruto la mwezi Juni kuondoa marufuku ya 2018 ya ukataji miti.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.