Pata taarifa kuu

Kenya: Mahakama yaongeza muda wa kusitisha kutumwa kwa Vikosi vya usalama Haiti

Mahakama kuu nchini Kenya, imeongeza muda wa kuzuia serikali kuwatuma polisi wake nchini Haiti kukabiliana na makundi ya magenge nchini humo.


Polisi wa kutuliza ghasia nchini Kenya wakati wa makabiliano na waandamanaji katika eneo la Kibera jijini Nairobi, Kenya mnamo Julai 19, 2023.
Polisi wa kutuliza ghasia nchini Kenya wakati wa makabiliano na waandamanaji katika eneo la Kibera jijini Nairobi, Kenya mnamo Julai 19, 2023. © Brian Inganga / AP
Matangazo ya kibiashara

Ni uamuzi unaojiri wakati huu umoja wa mataifa ukisema usalama nchini Haiti umedorora zaidi, ambapo makundi ya magenge yanathibiti baadhi ya miji.

Nchi ya kenya ilikuwa imejitolea kuongoza ujumbe wa umoja wa mataifa kudhibiti magenge hayo nchini Haiti, ila mwanasiasa wa upinzani Ekuru Aukot, akafika mahakamani kupinga hatua hiyo kwa misngi kuwa katiba ya Kenya hairuhusu polisi wake 1000, kutumwa nje ya nchi.

Bunge lilistahili kuidhinisha kutumwa polisi hao nchini Haiti, mawakili wa bunge la Kenya wamesema bunge haliwezi kujadili swala ambao lipo mbele ya mahakama.

Kenya ilichukuwa hatua ya kutaka kuwatuma wanajeshi wake kule haiti kutokana na wito wa waziri mkuu Ariel Henry, kutraka jamii ya kimataifa kuisadia nchi yake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.